Tuesday, February 28, 2012

WASHINDI WA SHINDANO LA ZAMU YAKO KUSHINDA WA KAMPUNI YA TIGO WAZAWADIWA

Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya tigo, Alice Maro kushoto
akikabidhi zawadi kwa mshindi wa lap top ,Flora Lyimo baada wa kuiibuka mshindi
wa promosheni ya zamu yako kushinda anaeshuudia katikati ni Mratibu wa
Promosheni na Matukio wa Kampuni ya tigo,Edward Shila
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Tigo, Alice Maro kushoto
akikabidhi mfano wa hundi kwa Fidelis Mosha baada ya kuibuka mshindi wa
promosheni ya zamu yako kushinda katikati ni Mratibu wa Promosheni na Matukio wa
Kampuni ya tigo, Edward Shila
Baadhi ya washindi wa promosheni ya zamu yako
kushinda inayoendeshwa na kampuni ya tigo wakiwa wameshika mfano wa hundi baada
ya kukabidhiwa leo

Monday, February 27, 2012

WAZIRI WA FEDHA APOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MAABARA

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Hadji Mponda (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), wakati akipokea vifaa vya Maabara vilivyotolewa na Taasisi ya Kijerumani ya MERCK, Dar es Salaam jana. Kulia ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Karl-Ludwing Kley.

MASHINDANO YA SAFARI RAGER NYAMA CHOMA














“SAFARI LAGER NYAMA CHOMA 2012” YATANGAZA BAA ZILIZOFANIKIWA KUINGIA FAINALI MBEYA.








Dar es Salaam, Jumatatu Feb 27, 2012: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza majina ya baa bora zilizochaguliwa kuingia kwenye hatua ya fainali mkoani mbeya baada ya mchujo wa awali kukamilika kwenye yale mashindano ya aina yake na ya kuvutia ya kuchoma nyama yajulikanayo kama “Safari Lager Nyama Choma 2012”






Akizungumza na waandishi wa Habari kwenye Hotel ya Kebby”s Jijini Dar es Salaam Jaji mkuu wa mashindano hayo Bwana Douglas Sakibu alisema baa zilizochaguliwa kuingia hatua ya fainali jijini Mbeya ni.New Cit park,2000 Grocery,Makasini Bar,Savoy Bar na Free Park Bar. ambazo sasa zinasubiri siku ya fainali kwenye uwanja wa CCM Ilomba jumapili ya 04/03/2012






Alisema baa na majiko hayo yatakutana hapo mapema na kufanya shindano la wazi ili kuweza kumpata bingwa wa jiji hilo na wananchi watapata nafasi ya kujionea namna nyama choma inavyoandaliwa katika kiwango cha hali yajuu kabisa.






Baa hizi zilizoingia hatua ya fainali zote zina kiwango cha hali ya juu kabisa na hakika wameonyesha ujuzi na uzoefu mkubwa jambo linaloashiria kuwepo kwa ushindani mkubwa hivyo ni vyema wakazi wa jiji La Mbeya na vitongoji vyake wakawahi mapema jumapili pale Ccm Ilomba na kupata wasaa wa kushuhudia namna nyama zinavyoandaliwa kwa uhodari mkubwa huku wakiwa na bia yao waipendayo ya Safari Lager.






Kwa upande wake meneja wa bia ya Safari lager ambao ndio waandaaji wa Mashindano hayo Bwana Oscar Shelukindo aliwataka wakazi wa jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi siku ya fainali na pia mashabiki wa baa hizo kuja kuzishangilia na kuziunga mkono baa zao ili ziweze kuibuka washindi, sambamba na hayo bado kutakuwa na burudani nyingi toka kwenye bendi mbalimbali zitakazotumbuiza siku hiyo ili kuweza kutoa burudani kwa washabiki na wakazi wa jiji hilo kuanzia majira ya saa tano za asubuhi, pia kutakuwa na zawadi mbalimbali kwa washabiki zitakazotolewa.






Tutaendelea kuwa karibu na wapenzi wetu wa vinywaji toka Tbl hususani wa bia yetu ya Safari kwa kuwapatia burudani mbalimbali,Nyama choma bomba zaidi huku wakipata nafasi ya kujishindia zawadi kibao hivyo ni shindano ambalo mtu hapaswi kukosa hata kidogo.






Wakati huo huo majaji wa mashindano hay oleo wanafanya semina na baa zilizofanikiwa kuchaguliwa jijini Dar Es Salaam kasha kesho kuanza mchakato rasmi wa kuzitembelea kwenye maeneo yao kwa nyakati tofauti ili kuweza kupata baa zitakazofanikiwa kuingia hatua ya fainali hivi karibuni




Semina ya leo inazishirikisha baa za Huduma bar,Rosehill garden,Kilwa Road Pub,Pentagon Pub,Texedo Garden,Gadafi Square,Angels Pub,Fyatanga Bar,Jambo Lee,Hongera Bar,Braek Point Bar,Meeda Bar,Titanic Bar,Mangi Bar,Africenter Bar,Kisuma bar na Twiga bar .






.Alisema hii ni fursa ya pekee kwa wachoma nyama na wenye mabaa kuweza kupata mafunzo yakinifu juu ya uandaaji na uchomaji wa nyama toka kwa wataalam wenye ujuzi na waliobobea kwenye taaluma hiyo ili kuweza kukuza na kuboresha biashara zao na hatimae kufikisha kwa wateja kitu kilichokuwa na ubora wa hali ya juu.




Mashindano ya Safari Nyama Choma mwaka huu yanafanyika kwa mara ya nne ambapo mwaka jana washindi wa Jiji la Dar Es Salaam walikuwa Kisuma Bar ya Temeke Mwembe Yanga,Mbeya walikuwa Mbeya Canival,Kilimanjaro walikuwa Makanyaga bar ya Soweto na Arusha walikuwa SongaMbele Bar ya Sakina.

AIRTEL YAWAZAWADIA WASHINDI WA “NANI MKALI” PROMOSHENI























· Washindi 7 wa kila siku na mshindi wa wiki wazawadi




27, Februari 2012 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayotoa huduma nafuu na yenye wigo mpana zaidi wa mawasiliano, leo imewazawadia washindi wa wiki ya kwanza ya promosheni ya nani Mkali pesa taslimu ambapo washindi wa kila siku wamekabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja na mshindi wa wiki ameondoka na shilingi milioni tatu. washindi hao wamepatikana kutoka katika mikoa mbalimbali Tanzania ikiwepo Mwanza, Tanga, Mbeya, Arusha na Dar es Saalam




Akiongea wakati wa kukabithi zawadi hizo Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde alisema” Airtel inawapa nafasi nyingine watanzania kushiriki na Kushinda fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 200,kwa washindi 110 watakaopatikana kila siku, kila wiki na kila mwezi katika promosheni yetu kabambe ya Nani Mkali. Na leo napenda kuchukua fulsa hii kuwatangaza washindi wa wiki ya kwanza ambao ni Bw Daniel Mshana , Dr. Hetal Anthan na Albogast Oiso wa Dar es saalam, wengine ni Said Seif wa Mwanza,Junior Pesambili wa Arusha na Abdi Ibrahim Mohamed wa Muheza Tanga hawa walijishindia million moja kila mmoja na ambapo bwana Abdi Ibrahim zaidi ya kuwa mshinidi wa siku ameibuka kuwa mshindi wa wiki na kuondoka na pesa taslim shilling million tatu”.




Tunaendelea kuwajali na kuwazawadia wateja wetu nchi nzima kuhakikisha washindi wengi wanapatikana, tunaendelea kuimarisha dhamira yetu ya kutoa huduma bora zenye viwango vya juu na kudhihirisha kauli mbiu yetu ya jisikie huru, aliongeza Matinde




kujiunga na “Nani Mkali”, mteja anatakiwa kuandika neno “Mkali” na kutuma kwenye namba 15656 bure kabisa. Baada ya hapo atatumiwa maswali na kila atakapo toa jibu sahihi atapata pointi 20 na jibu lisilo sahihi pointi 10.Kila ujumbe wenye jibu utatozwa shillingi 350 pamoja na

Ujio wa kipindi kipya cha TV "Ongea na Janet Tv Talk Show."!








Janet akirekodi kipindi na mmoja wa wadau wake aliyefika studio





Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV talk show pichani kulia akiwa na mmoja wa mwanasumbwi hapa nchini Japhet Kaseba akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.


Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV Talk Show pichani kulia akiwa na mmoja wa wadau akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.







Ongea na Janet ni Talk show ambayo inazungumzia mambo yanayotugusa katika maisha yetu ya kila siku,Inahusisha Jinsia zote na rika zote. Kipindi changu nilikitengeneza mwaka 2009 june 26 lakini bahati mbaya ilikuwa ni ngumu sana kupata airtime hasa ikizingatiwa ni kipindi toka nje ya kampuni husika,bado wahusika hawajakubali kubadilika ila hii "ishu" digital itasaidia sana. -Sijaajiriwa na Clouds Tv bali tumeingia Mkataba kama (partiners) .









Ni kipindi ambacho sitegemei kishuke bali kitakuwa kinapanda na watu wategemee mabadiliko,nimeanzia chini napanda juu katika kuleta changamoto,Natamani watu wenye talents wazitumie bila kuogopa na wasikate tamaa,kwa mfano,nimehangaika na kipindi changu kwa miaka mitatu na sasa ndio naanza kuona matunda ya uvumilivu,ubishi wa kutimiza ndoto na kutokukubali kushindwa kufikia malengo.









Wasijali maneno ya watu ya kukatisha tamaa,mtu asimame kwenye anachokiamini na akifanyie kazi haijalishi itachukua muda gani.Nategemea,kuelimisha,kushauri na kuburudisha.Niliacha kazi ITV 2008, alafu nikajiunga NGO ya Canada lakini damu yangu iko kwenye media...nimeamua kurudi na kuacha kila kitu nyuma. Nataka kukamilisha ndoto zangu zote zilizosimama kwa miaka 4.-Kipindi kinaanza tarehe 8 March,alhamis saa 3 kamili







Asanteni sana Wadau

TRA YAANZISHA MPANGO MPYA WA UKUSANYAJI KODI












NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE- ARUSHA


MAMLAKA ya mapato Tanzania(TRA)imeanzisha utaratibu wa ukusanyaji


kodi shirikishi kwa kutoa elimu ya mlipa kodi kwa wafanyabiashara nchi nzima,ikiwa ni mkakati wa kuongeza mapato ya serikali bila shuruti


Aidha mkakati huo ambao umeanzia katika mikoa ya kanda ya kaskazini,unalenga kuwafanya wafanyabiashara waelewe kuwa TRA ni rafiki ya mlipa kodi na kwamba kulipakodi bila shuruti ni wajibu kwa maendeleo ya taifa. Meneja wa mambo ya ndani ,ofisi ya kamishina mkuu wa TRAnchini,Bi Stela Cosmas aliyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na chama cha wafanyabiashara mkoani Arusha(TCCIA)


Cosmas aliwataka wafanyabiashara kufuata taratibu nakanuni za mlipa kodi ikiwemo kutoa stakabadhi zilizosahihi kwa wateja wao kuwasilishamalipo ya kodi sahihi,ritani sahihi, nyaraka za forodha na madai ya marejesho ,kutoa na kudai stakabadhi ankra za kodi .Aidha alito wito kwa wafanyabiashara kuepuka ukwepajikodi kwa kutumia risiti,ambapo alidai yakuwa wafanyabiashara wamekuwa na tabiaya kumwandikia mteja risiti yenyekiwango tofauti na iliyopo kwenye kitabu chake cha mauzo,kwani kwa kufanyahivyo ni kuinyima serikali mapato na ninikinyume cha sheria. Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya mapato mkoa wa Arusha,EvaristKileva alisema kuwa, wajibu wao kama TRA ni kuhakikisha kuwa wanahamasisha walipa kodi kulipa kodi kwa wakati kwa ajili ya manufaa ya watanzania kwa ujumla . Kileva alisema kuwa wadau wakuu wa TRA ambao niwalipa kodi wanapaswa kuhudumiwa kwa umakini mkubwa bila kuwepo kwa malalamikoyoyote kati yao na mamlaka husika ambapo alisema endapo kutakuwepo na kutokuelewanakati yao na wafanyakazi wa TRA wawakilishe malalamiko yao kwa meneja mwenyeweili yaweze kuchukuliwa hatua. Aliongea kuwa, ni vizuri walipa kodi wakawa na mahusianomazuri kati yao na mamlaka ya mapato ili kuboresha huduma zinazotolewa bilakuwepo kwa vikwazo vya aina yoyote ikiwa ni pamoja na walipa kodi kujijengea tabia ya kuwasilisha malalamiko kwa wakati na kwa mamlaka hiyo na sio nje yahapo huku lengo hasa likiwa ni kuendelea kudumisha mahusiano mazuri . ‘’ndugu zanguwafanyabiashara ofisi yetu ipo wazi kila siku kwa ajili yenu tafadhili kamakuna matatizo yanajitokeza msikumbatie malalamiko leteni ofisini’’alisema Bw Kileva Alisema kuwa, elimu hiyo imeweza kuwanufaisha kwa kiasikikubwa sana kwani hapo awali walikuwa hawana uelewa wowote jinsi ya kuwahojiwatendaji wa TRA pindi wanapofika katika maeneo yao kwa ajili ya kudai kodi Alifafanua kuwa kupitia mafunzo hayo yamewawezesha kwakiasi kikubwa sana kuwa na mahusiano mazuri kati yao na mamlaka hiyo ,pamoja nawatendaji wa mamlaka kwa ujumla kwani wataweza kufanya kazi kwa ushirikiano wahali ya juu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Waziri Tibaijuka akabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano ya NBC Lady Captains’’ Trophy 2011.









Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi aliyepiga umbali mkubwa zaidi, Vivienne Mwaulambo wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi. Katikati ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale ambaye benki yao ilidhamini mashindano hayo.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi wa jumla wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011, Halima Makame yaliyodhaminiwa na Benki ya NBC Katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi wa tatu wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011, Violet Peter katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi.


Mmoja wa viongozi wa DGC kitengo cha gofu ya wanawake, Joyce Srvarva (kulia) akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale kwa kutambua mchango wa benki hiyo kufanikisha mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 katika viwanja hivyo juzi


Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (wa pili kulia) akipiga picha ya kumbukumbu na viongozi wa kitengo cha gofu ya wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam, mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na NBC katika viwanja hivyo juzi. (Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale

Sunday, February 26, 2012

MSONDO NGOMA YAFANYA MAKAMUZI UKUMBI WA MAX BAR LEO




Waimbaji wa Bendi Kongwe ya Msondo Ngoma wakitoa burudan katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni Jumapili hii kutoka kushoto ni Hasani Moshi TX JR,Eddo Sanga na Juma Katundu.(Picha na www.burudan.blogspot.com)

Wasanii wa bendi ya msondo wakitumbuiza katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni mpiga gita la RIDHIM, Mustafa Pishuu na mpiga tumba Amiri Said Dongo.(Picha na www.burudan.blogspot.com)




Waimbaji wa Bendi ya Msondo ngoma Baba ya Muziki wakitoa burudan wakati wa onesho lao lililofanyika katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni Shabani Dede na Juma Katundu.(Picha na www.burudan.blogspot.com)



Wapuliza Saxsaphone wa bendi ya Msondo ngoma wakiwajibika wakati wa onesho lao lililofanyika katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni Hamisi Mnyupe na Romani Mngande Romariooo.(Picha na www.burudan.blogspot.com)

MBIO ZA VODACOM 5KM FUN RUN ZAFANA NDANI YA KILI-MARATHON MJINI MOSHI










Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 80,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa tatu upande wa wanawake Natalia Elisante, wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.



Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 80,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa pili wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.


Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 100,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa kwanza upande wa wanawake Jackline Sakilu, wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.


Baadhi ya washindi wa Vodacom 5 KM fun run wakiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Rukia Mtingwa kulia na Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude kushoto.




Ofisa Masoko Mkuu na Mahusiano akishiriki katika mbio za kujifurahisha za”Vodacom 5 KM fun run”




Mmoja wa washiriki walemavu alieshiriki katika mbio za kujifurahisha za “Vodacom 5 KM fun run”akimaliza mbio zake.




Baadhi ya washiriki wa mbio za kujifurahisha za”Vodacom 5 KM fun run”wakimaliza mbio zao nakujinyakulia zawadi mbalimbali.


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Rukia Mtingwa wa pili toka kushoto akifurahia jambo na baadhi ya watoto wenye ugonjwa wa ukimwi mara walipomaliza kushiriki katika mbio za kujifurahisha za “Vodacom 5 KM fun run”

MASHINDANO YA NBC LADIES GOLF SECTION YAFANYIKA LEO GYMKANA CLUB

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC, Mwinda Kiula-Mfugale akijiandaa kupiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni wachezaji na maofisa wa NBC.






Nahodha wa DGC Ladies Golf Section, Vivienne Mwaulambo akipiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale, baadhi ya wachezaji na maofisa wa benki hiyo.


: Mcheza gofu, Halima Mussa akipiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na NBC jijini Dar es Salaam leo

Saturday, February 25, 2012

MATUMLA AMSAMBALATISHA MTAMBO WA GONGO

)
Refarii Antoni Luta katikati akimnyoosha mkono juu bondia Rashidi Matumla Snake Man kuashiria ushindi dhidi ya mpinzani wake maneno Osward Mtambo wa Gongo kushoto wakati wa mpambano wao uliochezwa Jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Matumla alishinda kwa point.(Picha na http://www.superdboxingcoach.blogspot.com/




Mabondia Maneno Osward Mtambo wa Gongo (kushoto) na Rashid Malumla Snake Man Wakioneshana umwamba wa kutupa masumbwi wakati wa mpambano wao uliochezwa Jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Matumla alishinda kwa point.(Picha na www.superd boxingcoach.blogspot.com)

Date: 2012-02-25Venue: PTA Hall, Dar es Salaam , TanzaniaCommission: Pugilistic Syndicate of TanzaniaPromoter: Issa Malanga Promotion [1] Lightfly weight Moses Musa WPTS 4 rounds of a 4 rounder VS Fred Cloud- Referee: Ramadhan Basta 39 - 37 [2] Super Featherweight 6 roundsShomari Mirundi DREW 4 rounds of a 4 rounder VS Mohammed Kashinde- Referee: Pembe Ndava 38 - 38 [3] Super Bantamweight 4 roundsMuhidini Ndolanga WPTS 4 rounds of a 4 rounderVS Shukuru Said- Referee: Ramadhan Basta 40 - 36 [4] Light Welterweight Hamis Mputeni WKO round 2 of a 6 rounder VS Rashid Makali- Referee: Pembe Ndava; Judges:Ramadhan Basta, Emmanuel Mlundwa, Anthony Ruta [5] Flyweight 6 roundsHassani Kiwale WTKO round 2 of a 6 rounder VS Mawazo Kanju- Referee: Emmanuel Mlundwa Judges: Pembe Ndava , Ramadhan Basta, Anthony Ruta [6] Super Middleweight 6 roundsIdd Kigula WTKO round 4 of a 6 rounder VS Shabani Kaineko- Referee: Emmanuel Mlundwa Judges: Pembe Ndava , Ramadhan Basta, Anthony Ruta [7] Female Boxing Middle/Super MiddleMonica Mwakasanga WPTS 4 rounds of a 4 rounder VS Furaha Nganda - Referee: Emmanuel Mlundwa 40 - 36 [8] Super Middleweight 10 roundsRashid Matumla WPTS 10 rounds of a 10 rounder VS Maneno Oswald- Referee/Judge: Anthony Ruta 97 - 93; Judges: Pembe Ndava 95 - 95, Ramadhan Basta 97 – 95

RASHIDI MATUMLA VS MANENO OSWARD KUPAMBANA TENA LEO FEBRUARY 25 UKUMBI WA PTA SABASABA DAR...!!!
















MAANDALIZI ya pambano lisilo la ubingwa kati ya mabondia Rashid
Matumla ‘Snake Man’ na Maneno Oswald ‘Mtambo wa Gongo’ lililopangwa
kuwa Februar 25 mwaka huu leo yanaenda vizuri.Promota wa mpambano huo Issa
Malanga, alisema pambano hilo limeandaliwa ili kumaliza ubishi baina
ya mabondia hao, ambao pambano la mwisho walitoka sare ya point 99.99

Hata hivyo Oswald aliwalalamikia majaji kuwa hawakumtendea haki.
Mabondia hao wamewahi kupambana mara nne, Oswald akishinda mara moja
na Matumla mara mbili na kutoka sare mara moja.

Alisema pambano hilo linatarajia kuwa la raundi 10 uzito wa kati,
litafanyika kwenye ukumbi wa PTA sabasaba Dar es salaam


Mpambano huo wa kumaliza ubishi baada ya kila mmoja wao kudai
alishinda katika mpambano wao wa mwisho

Aidha aliwataja wakali watakaosindikiza mpambano huo ni Shomali
Mirundi na Mikidadi Abdallah 'Tatson', na Iddy Mkenye atapambana na
Shabani Mtengela ' Zunga Boy', Abdallah Mohamedi na Saleh Mkalekwa
mbali na hayo mpambano mwingine ni Ramadhani Mashudu na Hassani Kiwale
'Moro Best

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye
mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Roy Jonas,Evander holyfield,Lenox Lewis, Manny Paquaio, Floyd Maywherth,
Roy Jones na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali
ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila
‘Super ‘D’.
“Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika
pambano la Cheka na Maugo ili kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni
pamoja na sheria za mchezo wa ngumi,” alisema Super ‘D’

MAMA ASHA BILAL ATEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA KATANDALA SUMBAWANGA














Mke Wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akisalimiana na mmoja kati ya watoto Yatima, Juma, baada ya kuwasili kwenye Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Katandala kilichopo Sumbawanga jana Februari 24, 2012 kwa ajili ya kukabidhi Tanki la kuhifadhia maji la Lita 5000 katika kituo hicho. Picha na Muhidin Sufiani-OMR



Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akisalimiana na mfanyakazi wa kujitolea kutoka nchini Ujerumani, Liza Gernemann, aliyembeba mtoto William wa Kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Katandala, wakati alipofika katika kituo hicho jana Februari 24, 2012 kwa ajili ya kukabidhi Tanki la kuhifadhia maji la Lita 5000. Picha na Muhidin Sufiani-OMR



Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akiwa amembea mmoja kati ya watoto Yatima wanaolelewa katika Kituo cha kulelea watoto hao katika Kituo cha Katandala, wakati akitembelea katika vyumba vya kulala vya watoto hao, alipofika kukabidhi Tanki la maji la Lita 5000 kituoni hapo jana Februari 24, 2012. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Sumbawanga na Katavi, Eng. Stella Manyanya. Picha na Muhidin Sufiani-OMR



Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, kishikana mkono na Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Katandala, Sr. Maria Goreth Chusu, ikiwa ni ishara ya kumkabidhi Tanki la kuhifadhia maji la Lita 5000 katika kituo hicho alipofika kituoni hapo kilichopo Sumbawanga jana Februari 24, 2012. Kushoto kwa Mama Asha ni Mkuu wa Mkoa wa Sumbawanga na Katavi, Eng. Stella Manyanya (kushoto) ni Sr. Scolastica Mwembezi. Picha na Muhidin Sufiani-OMR


MAMA MARIA NYERERE AWAASA WAKE WA VIONGOZI














MKE WA HAYATI Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere amewataka wake wa viongozi kutambua dhamana walizonazo na wajibu walionao kwa jamii ambayo wenzi wao wanaiongoza.








Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumamosi, Februari 25, 2012) wakati alipokuwa akiwashukuru wake wa viongozi 25 ambao walifika nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam ili kumjulia hali na kumpa tuzo ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.








Mama Maria amesema kuwa wake wa viongozi kunawafanya wakutane na changamoto nyingi lakini pia akawataka watambue kuwa Taifa limewapa fursa ya kuelewa mengi ambayo kama wangekuwa wanawake wa kawaida tu wasingeweza kujua mambo hayo.








“Unapokuwa mke wa kiongozi unapata changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kutoa dira kwa wengine... unapaswa kufikiri kwa niaba ya wengine iwe ni kwenye ujasiriamali, elimu, afya au masuala ya kijamii hasa namna ya kukabili changamoto za akinamama na watoto,” alisema.








“Unapokuwa mke wa kiongozi unapaswa kumshukuru kwa kuwa umepewa fursa ya kuwaongoza wengine, umepewa fursa ya kukomaa na mawazo yanakua kwa haraka kule wengine wasio na fursa kama yako,” alisisitiza.








Alisema inawezekana watu wa nje wakawaonea wivu kuwa wamepata bahati ya kuolewa na viongozi lakini wajibu wao mkubwa siku zote uwe ni kuwaombea wenzi wao na wale wanaowaongoza. “Msichoke kumuomba Mungu kwa sababu ninyi ndiyo mna kazi kubwa, mnasimama kwa niaba ya Taifa... lolote likitokea linawakumba na ninyi pia,” aliongeza.








Mapema, akitoa salamu za ujio wao, mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda alisema wameamua kumpa tuzo ya heshima Mama Maria Nyerere kwa sababu wanatambua mchango wake wakati aliposhiriki bega kwa bega na hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwenye harakati za uhuru wa Tanzania.








Akizungumza kwa niaba ya wake wa viongozi mbalimbali wa kitaifa 25 ambao aliongozana nao, Mama Pinda alisema tuzo waliyompa imeandikwa “Hongera Mama wa Taifa” ikiwa ni kuthamini mchango wake. Tuzo hiyo ina umbo la ramani ya Tanzania, ina nembo ya miaka 50 ya Uhuru pamoja na picha ya Mama Maria Nyerere.












Baadhi ya wake wa viongozi walioambatana Mama Pinda ni wake wa Marais wastaafu Mama Sitti Mwinyi na Mama Anna Mkapa, Mke mkubwa wa Makamu wa Rais, Bi. Zakia Bilal, Mama Salma Omar (mke wa marehemu Dk. Omar Ali Juma), Mama Hasina Kawawa, na wake wa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu wakuu

Friday, February 24, 2012

EXTRA BONGO WAONGEZA NGUVU TENA.

Kikosi cha mbele kilichobomolewa Stone Mayasika

a Michael Machellah
MKURUGENZI wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Chocky ameibomoa safu ya

mbele ya Bendi ya Stone Mayasika.

Akizungumza na mtandao huu Chocky alijijitea kuwa si yeye aliyefanya hivyo

bali ni wacheza shoo wenyewe wameamua kuihama kwa mapenzi yao na maslahi

yao binafsi.

Wakizungumza na mtandao huu walisema ukweli kuwa Extra Bongo iko

juu,kuanzia kwenye jina huwezi kuilinganisha na Stone Mayasika,pili Extra

Bongo ina wapenzi wengi ukilinganisha na Stone Mayasika,tatu ni bendi

inayoongoza kwa sasa katika Bendi za muziki wa Dansi na mwisho ni maslahi

ndio yaliyowatoa Stone Mayasika kwenda Extra Bongo.

Kiongozi wa wacheza shoo, Super Nyamwela alisema ni kweli wacheza shoo hao

wapo na tayari wameshaanza kucheza wakati wakiwa kambini kufundishwa

yaliyopo na yanayojili Extra Bongo.

Extra Bongo leo watakuwa viwanja vya Kijichi,kesho jumamosi ni katika

Uwanja wa Nyumbani Meeda Sinza Dar es Salaam na jumapili ni Dar Live

MABONDIA MANENO OSWARD NA RASHIDI MATUMLA KUMALIZA UBISHI KESHO FEB 25 UKUMBI WA PTA SABASABA



Mabondia Furaha Nganda na Monica Mwakasanga wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito leo

Bondia Furaha Nganda akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake utakaofanyika jumamosi feb 25 na bondia Monica Mwakasanga kushoto kulia ni Katibu wa Shilikisho la ngumi za Kulipwa Tanzania PST Anton
Bondia Maneno Osward akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake utakaofanyika katika ukumbi Wa PTA sabasaba jumamosi ya Feb 25 (kushoto) ni mpinzani wake Rashidi Matumla kulia ni katibu wa PST, aNTON Luta.(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Bondia Shabani Kaineko akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Antoni Mwakapalila utakaofanyika katika ukumbi wa PTA sabasaba kesho kulia ni Katibu wa Shilikisho la ngumi za Kulipwa Tanzania PST Anton Luta(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Mabondia Antoni Mwakapalila akitunishiana misuri na bondia Shabani Kaineko baada ya kupima uzito leo kwa ajili ya mpambano wao wa kirafiki utakaofanyika Kesho katika ukumbi wa PTA Sabasaba(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA MAGHARALA MAWILI YA KUHIFADHIA BIDHAA KTK BANDARI YA KASANGA NA KUTEMBELEA WAFANYA BIASHARA WA SAMAKI



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika moja ya jengo kati ya mawili ya Maghala ya kuhifadhia Bidhaa yaliyopo katika Bandari ya Kasanga, kijiji cha Lusambo Wilaya ya Sumbawanga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Luteni Godfrey Semiono (Mkuu wa Kambi) kukagua kikosi cha Ulinzi wa Mipaka cha Kasanga kilichopo katika kijiji cha Lusambo, pembezoni mwa Wilaya ya Sumbawanga, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuzindua maghala ya kuhifadhia bidhaa katika Bandari ya Kasanga jana Februari 23, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki katika Soko la Samaki la Kasanga, baada ya kuweka jiwe la msingi katika soko hilo akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa, jana Februari 23, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kuwaaga wananchi wa Kijiji cha Lusambo waliojitokeza katika mapokezi yake alipofika kuweka jiwe la msingi katika Soko la Kasanga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

BENDI YA MACHOZI YA LADY JAY DEE YAPATA NEMBO YA BIDHAA BARCODES

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi (TPSF), Godfey Simbeye (kulia) akimkabidhi Gadna Habash kiongozi wa Bendi ya Machozi, ya Judith Wambura Lady Jay Dee, nembo ya mistari ya bidhaa BARCODES katika hafla iliyofanyika, Dar es Salaam. Nembo hiyo imetengezwa na kampuni ya GSI
Gadna akizungumza baada ya kupokea nembo hiyo ya biashara
Gadna (wa pili kulia) akionesha moja ya albamu ya nyimbo za bendi ya machozi ambayo ina nembo hiyo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi (TPSF), Godfey
Wafanyakazi wa kampuni ya GSI wakiwa katika picha ya pamoja na Gadna Habash
Gadna akibadilishana mawazo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi (TPSF), Godfey Simbeye (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Uanachama wa TPSF, Louis Accaro