Pages

On 0 comments

  Mabingwa wa mchezo wa Pool Mkoa wa Dar es Salaam,CBE wakishangilia na kitita cha sh.500,000  mara baada ya kuibuka washidi katika mashindaano hayo yajulikanyo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.
Bingwa Mtetezi wa mashindano ya Pool yajulikayo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mkoa wa Dar es Salaam na Taifa, Peter Patrick akiwa amebebwa na mashabiki mara baada ya kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Dar es Saalaam tena wakati wa mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.
 
Na Mwandishi Wetu
CBE Dar na SAUT Mwanza mabingwa Safari Pool
MABINGWA watetezi wa Mkoa wa Mwanza na Taifa wa mashindano ya Pool,Chuo kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza(SAUT), juzi walifanikiwa  kutwaa ubingwa  wa Mkoa wa  mashindano ya mchezo wa pool kwa wanafunzi wa elimu ya juu mkoani Mwanza  yajulikanayo kama 'Safari Lager Higher Learning Competition 2013'  baada ya kuibuka na ushindi  dhidi ya Chuo kikuu cha CBE yaliyofanyika katika Klabu ya Villa Park jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.
Mashindano hayo yaliyoshirikisha vyuo vikuu vinne vya mkoani hapo ambavyo ni CBE,TIA,BMC na mabingwa SAUT kwa udhamini wa Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia kinywaji chake cha Safari Lager.
Chuo kikuu cha SAUT kwa kutetea  ubingwa  huo kilijinyakulia fedha taslim Sh.500,000 pamoja tiketi ya kuwakilisha mkoa Mwanza katika fainali za taifa zinazotarajiwa kufanyika Juni mosi mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na chuo cha CBE ambacho kilijinyakulia kitita cha Sh.300,000.Nafasi ya tatu ilichukuliwa na chuo cha BMC ambacho kilizawadiwa Sh.200,000 na nafasi ya nne ni Chuo Kikuu cha TIA ambacho kilipata Sh.100,000.
Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume), Vitalis Bakilane wa CBE aliibuka kuwa bingwa hivyo kujinyakulia pesa taslimu Sh.150,000 pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa kwa upande wa wachezaji mmoja mmoja.Nafasi ya pili ilichukuliwa na Joseph Sipamba wa SAUT ambaye alizawadiwa Sh.100,000.
Na kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake), Agnes Jacob wa CBE alitwaa ubingwa huo na kuzawadiwa pesa taslim sh.100,000 pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa katika mashindano ya kitaifa.Nafasi ya pili ilichukuliwa na Beatrice Benignus wa TIA ambaye alizawadiwa pesa taslim Sh 50,000.
Wakati jijini Dar es Salaam CBE walifanikiwa kumnyang’anya ubingwa wa Mkoa IFM, na kwa nafasi hiyo CBE ilijinyakulia kitita cha Shilingi 500,000 pamoja na tiketi ya kushiliki mashindano ya kitaifa . huku nafasi ya pili ikishikiliwa na IFM ambao walijinyakulia kitita cha Shlingi 300,000.
Nafasi ya tatu ilichukuliwa na ARDHI ambao walizawadiwa pesa taslimu sh.200,000 na nafasi ya nne ilichukuliwa na ROYAL ambao walizawadiwa pesa taslimu sh.100,000.
Upande wa wachezaji mmoja mmoja wanaume Bingwa mtetezi wa Mkoa na Taifa, Peter Patrick wa chuo cha IFM,alitetea ubingwa wake na kuzawadiwa pesa taslimu sh.150,000 pamoja na tiketi ya kushiriki mashindano ya kitaifa hapo juni mos jijini Dar es Salaam na nafasi ya pili ilichukuliwa na Saleh Amir wa IAMCO ambaye alizawadiwa pesa taslimu sh.100,000,wakati upande wa kinadada nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Lilian Meori na kujinyakula pesa taslimu sh.100,000 na tiketi ya kushiriki mashindano ya kitaifa wakati nafasi ya pili ilichukuliwa na Mariam Martman na kujinyakula pesa taslimu sh.50,000. 
 
 

On 0 comments

  Nahodha wa timu ya Chuo cha St.Augustine (SAUT),Jimy Nikas akionyesha kitita cha sh.500,000 mara baada ya chuo hicho kutetea ubingwa wa mashindano ya Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mwanza yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Villa Park.
Bingwa  wa mashindano ya Pool yajulikayo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mwanza,  Vitalis Bakilane akiwa amebebwa na mashabiki mara baada ya kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Dar es Saalaam tena wakati wa mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Villa Park jijini Mwanza.

On 0 comments




On 0 comments



Bonia Daudi Muhuzi akishindana na Mbuyu wa timu ya TASWA FC Majuto Omari wakati wa mpambano wao
Kocha wa kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila ' Super D' akisisitiza jambo wakati wa mapumziko
Mchezaji wa timu ya Taswa akipambana na bondia kuwania mpira
SUPER D BOXING COACH AKISISITIZA JAMBO WAKATI WA MAPUMZIKO WA MCHEZO HUO

On 0 comments

.




                                                      Press Release
TAMASHA la Mastaa chipukizi la mwezi Mei litafanyika tarehe 26 katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 10 jioni.

Vikundi vya sanaa vya Kaole, Splendid, Super Shine Taarab, Five Star Modern Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na Sarakasi wamethibitisha kushiriki tamasha hilo.

Wasanii wakongwe wa bongo flava kama Stara Thomas, Bendi ya Msondo Ngoma na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa.

Kauli Mbiu ni Kilio cha Msanii, wasanii wote wapendao kushiriki wafike ofisi za Splendid Ilala ili kujisajili.

SHIWATA pia inawapongeza wote walioshiriki tamasha  la Aprili 27 ambako zaidi ya wasanii 300 walishiriki kuonesha vipaji vyao ambako mgeni rasmi mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kutoka Wilaya ya Kinondoni, Calist Lyimo aliwaasa wasanii kujituma kuonesha uwezo wao katika kuelimisha jamii.

Pia Shiwata imeupongeza uongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab,vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau bwote tushirikiane katika matamasha haya ili kujenga ushirikiano wa pamoja.

Maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika ambako wasanii kutoka vikundi mbalimbali wamepiga kambi ya kujifua ili kuonesha ubunifu wao katika tamasha hilo.

Wakati huo huo SHIWATA inatarajia kuhamisha tamasha hilo kwa mwezi Juni kufanyikia mkoa wa Arusha ili kuwapa nafasi wasanii wa mkoa huo nao kuonesha uwezo wao.

Peter Mwenda 
Ofisa Habari wa SHIWATA
0715/0752-222677

On 0 comments






 

Tanzania imetengeneza historia mpya kwenye ngumi za kulipwa nchini Thailand baada ya mabondia wake kuwa wanapigwa kila mara wanapokwenda kuiwakilisha nchi na bara la Afrika. Safari hiiJEMBE, kijana mtanashati anayeinukia kwenye masumbwi Jonas Segu kutoka katika ukumbi wa mazoezi waRespect Gym Boxing Club ya Mabibo Loyola chini ya kocha Christopher Mzazi ameonyesha kipaji kikubwa cha kusukuma msumbwi alipoushangaza umati wa maelfu ya wananchi wa Thailand pamoja na nchi za ukanda wa Indo-China.
Segu alikuwa anachuana na bingwa wa IBF katika mara la Asia Pacific Patomsuk Pathompothong kutoka Thailand katika uzito wa Light Welter ambaye ni bondia namba 7 duniani katika viwango vya IBF. Mpambano wao ulifanyika katika jiji lenye mahekalu ya dhahabu la Bangkok na kurushwa na television katika nchi zote za ukanda wa Indo-Chinaza Laos, Myanmar, Cambodia, Vietnam na Thailand yenyewe.
Mpambano wa Segu na Pathompothong ulianza kwa bondia wa kitanzania kuchomoka kama upinde kwenye kona yake na kumshambulia Pathompothong kwa makonde mazito ya kumshikisha adabu. Segu alitupa makonde ya mchanganyiko na kumzidi Pathompothong kutokana na uzito na umakini wa ngumi zake. Kwa kipindi chote cha raundi ya kwanza ilimbidi Pathompothong ajilinde na kukimbia akizunguka ndani ya ulingo ili kudhoofisha masumbwi yaSegu aliyekuwa anayachanganya kama mashine ya kukomboa mpunga ambao unalimwa kwa wingi nchini Thailand!

Jonas Segu alikuwa chini ya uangalizi makini wa bondia maarufu mstaafu George “Lister” Sabuni ambaye aliweza kumpa maelekezo ya nini cha kufanya kwenye mpambano huo wa mwaka. Katika raundi ya 2, 3 na 4 Segu aliuonyesha umati wa mashabiki wa Thailand kuwa yeye kweli ni bingwa mtarajiwa na hakwenda Thailand kula wali wao ila kuiwakilisha nchi yake ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Segu alimhenyesha Pathompothong vilivyo kwa kumchakaza kwa makondde mfululizo hususan akiutumia mkono wake hatari wa kulia ambao ulionekana dhahiri kuwa unaleta madhara makubwa kwa Pathompothong.
Ilididi timu ya wataalam wa Pathompothong kutafakari namna ya kumdhibiti kijana huyo wa Kitanzania ambaye kweli alionekana kuwa alienda Thailand kuuchukua mkanda wa IBF Pan Pacific na sio kufuata ulaji! 
Raudi ta 5 Pathompothong aliingia ulingoni akiwa mtu tofauti kabisa akirusha msumbwi mfululizo na kutembea ulingoni kama siafu huku akimvuta Segu kenye kamba ili amkandamizie masumbwi yake. Kijana huyo nadhifu wa kitanzania (mwenye sura nzuri ya kuvutia na ambaye wasichana wengi wa Thailand walishinda karibu na hoteli aliyoshukia ili kuweza kuongea naye) alitumia wakati huo kumwonyesha Pathompothong kuwa yeye hababaishwi na masumbwi yake kwani amefanya mazoezi ya kutosha. Segu alibadilishana masumbi na Pathompothong vilivyo na kuufanya umati wa mashabiki waliojazana kwenye ukumbi huo kumshangilia kama vile yeye ndiye bondia wao wakiimba Tanzania, Tanzania, Tanzania!
Katika raundi ya 6 mabondia wote waliingia ulingoni kama vifaru na kubadilishana masumbwi ya mchanganyiko (combinations) wakitafuta kudhibiti harakati za mpinzani mwenza. Ni katika kubadilishana huku kwa masumbwi ambako Segu aliumizwa mkono na Mthailand Pathompothong. Inawezekana kuwa ni katika juhudi za kumzuia ili asiendelee kurusha masubwi ya nguvu na kudhoofisha nguvu zake.
Kuumia mkono kwa Segu ilikuwa dhahiri kwani mwanzoni mwa raundi ya saba wakati Pathompothong alipokuwa anamiliki ulingo dhidi ya kijana huyo mtanashati wa kitanzania. Katikati ya raundi ya saba Segu aliona kuwa hawezi kuutumia mkono wake vizuri na kumwashiria refarii wa mpambano kuwa anaacha!
Segu aliacha pambano hilo katika raundi ya saba wakati mashabiki wengi katika ukumbi huo wakiwa wanaimbaTanzania, Tanzania, Tanzania kwa jinsi alivyokuwa anapeperusha vyema bendera ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”

On 0 comments



Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.
Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.
Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.
Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.
Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.
Diamond akifanya makamuzi sambamba na kundi lake.
Ney wa Mitego akilishambulia jukwaa la Dar Live.
Mashabiki wakiburudika wakati wa shoo hiyo ndani ya Dar Live.
Diamond na kundi lake katika pozi kabla ya makamuzi.
DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar. (PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY/GPL)

On 0 comments





Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam hivi karibuni.

 
Vikipigwa marufuku viroba tutarudi kunywa gongo
Na Mwandishi Wetu.

BAADHI ya wananchi jijini Dar es Salaam, wamelalamikia hoja iliyozuka bungeni wiki hii kwamba kinywaji cha Konyagi aina ya Kiroba kipigwe marufuku nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao, walisema endapo serikali itachukua uamuzi wa kupiga marufuku kinywaji hicho, watarudia kunywa pombe aina ya gongo ambayo ni hatari kwa afya zao.

Mkazi wa Mbagala, Faustine Mwiruka aliyekutwa kwenye baa ya Kisuma, aliiasa Serikali kutothubutu kukubali kinywaji hicho kupigwa marufuku, kwani ikifanya hivyo wengi wa wananchi wenye kipato cha chini wataanza tena kunywa gongo na pombe za kienyeji.

Itabidi tufanye kama Zambia  ambao wamezuia viroba, lakini nchi nzima imejaa viroba vya Malawi, Zaire na Burundi, lazima tuiadhibu serikali ikose kodi kote kote, bia hatunywi, viroba vya nje tutakunywa, pamoja na gongo.


Alisema haingii akilini kukihusisha kinywaji hicho na ajali za magari, akidai kuwa hata kabla ya viroba kuingia sokoni ajali zilikuwepo nyingi.

"Sisi tuna imani na viroba kwa vile vina ubora wa uhakika tofauti na pombe ya gongo ambayo inapikwa bila kupimwa ubora hivyo ni hatari kwa usalama wa afya zetu." alisema Mwiruka.

Naye Ali Hassan mkazi wa Kinondoni kwa Manyanya, alisema, wanaotaka viroba vipigwe marufuku hawawatendei haki wananchi wa kawaida ambao kwa asilimia kubwa hawana uwezo wa kununua bia ambazo bei yake ni kubwa.

Mwandishi wetu aliyetembelea maeneo ya Ilala Kota Mchikichini alifanikiwakuhojiana na wakazi wa eneo hilo ambao wengi wao walisema kuwa jambo hilo lililozushwa wiki iliyopita wanaamini ni njama za wafanya biashara toka nchi jirani ambao hawaitakii mema Tanzania  kwa kuwa pombe hiyo kuwepo kwake pia kunakuza pato la Taifa.

Juma Pingu alisema kuwa haoni sababu ya kupiga marufuku viroba kwakuwa ni pombe ya wanyonge na kuwataka wabunge kuthamini bidhaa za nyumbani kwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari mwanzoni mwa wiki hii, Mkurungenzi Mkuu wa Konyagi, David Mgwassa alisema kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwa na mchezo mchafu wa kuharibiana jina sokoni kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari vya hapa nchini, kampeni inayoendeshwa na makampuni yenye uhusiano na makampuni makubwa ya pombe duniani yasiyo penda, nchi za afrika zizalishe pombe zake, bali ziendeleee kununua kutoka Ireland, wales. Kenya  and uingereza.

Wadau hao wa Pombe nchini walifikia uamuzi wa kutoa maoni hayo baada ya kuona kuwa kinywaji chao Kiroba kinapigwa vita lukuki kwenye magazeti. Huwezi ukahusisha viroba na piki piki, kwani nchi hii ina piki piki laki tatu, na wananchi million 43, uhusiano wake uko wapi, kwanza hata leseni hamuwapi?

On 0 comments

.



Kiwanja Kinauzwa  kipo mbezi salasala Ukubwa ni Mita 26 KWA 21 Bei ni milioni 15 kwa maelezo zaidi wasiliana na Ngaeje 0713873412

On 0 comments

.






Maofisa wa Jeshi kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha Ghana, wakitembelea Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dar es Salaam, kwa lengo la kujenga ushirikiano katika nyanja za Sayansi, Teknolojia, Kiuchumi na Kijamii.Maofisa wanaosoma katika chuo hicho wanatoka Afrika Kusini, Nigeria, Ivory Coast, Togo, Rwanda na Ghana. (PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Meneja Uhusiano wa TBL, Doris Malulu (kulia) akitoa maelezo kwa maofisa hao kuhusu shughuli mbalimbali za kampuni hiyo.
Maofisa wa Jeshi wakitembelea kiwanda hicho
 Maofisa wa Jeshi wakipata maelezo jinsi bia inavyopikwa kwa kutumia kompyuta
Maofisa wakiwa na baadhi ya watalaamu wa maabara ya TBL
Add caption
 Mpishi wa Bia wa TBL, Kelvin Nkya akiwaeleza maofisa hao jinsi bia inavyochachuliwa
 Meneja wa Kiwanda cha Bia cha TBL Dar es Salaam, Calvin Martine (kushoto) akimkabidhi zawadi
Maofisa wa Jeshi wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa TBL baada ya kumaliza ziara.