Mabingwa wa mchezo wa Pool Mkoa wa Dar es Salaam,CBE wakishangilia na kitita cha sh.500,000 mara baada ya kuibuka washidi katika mashindaano hayo yajulikanyo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.
Bingwa
Mtetezi wa mashindano ya Pool yajulikayo kama Safari Lager Pool Higher Learning
Pool Competitio 2013 Mkoa wa Dar es Salaam na Taifa, Peter Patrick akiwa
amebebwa na mashabiki mara baada ya kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Dar es Saalaam
tena wakati wa mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza
jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi
Wetu
CBE Dar na
SAUT Mwanza mabingwa Safari Pool
MABINGWA watetezi
wa Mkoa wa Mwanza na Taifa wa mashindano ya Pool,Chuo kikuu cha Mtakatifu
Agustino Mwanza(SAUT), juzi walifanikiwa kutwaa ubingwa
wa Mkoa wa mashindano ya mchezo
wa pool kwa wanafunzi wa elimu ya juu mkoani Mwanza yajulikanayo kama 'Safari Lager Higher
Learning Competition 2013' baada ya
kuibuka na ushindi dhidi ya Chuo kikuu
cha CBE yaliyofanyika katika Klabu ya Villa Park jijini Mwanza mwishoni mwa
wiki.
Mashindano hayo
yaliyoshirikisha vyuo vikuu vinne vya mkoani hapo ambavyo ni CBE,TIA,BMC na
mabingwa SAUT kwa udhamini wa Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia kinywaji
chake cha Safari Lager.
Chuo kikuu cha SAUT
kwa kutetea ubingwa huo kilijinyakulia fedha taslim Sh.500,000
pamoja tiketi ya kuwakilisha mkoa Mwanza katika fainali za taifa zinazotarajiwa
kufanyika Juni mosi mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Nafasi ya pili
ilichukuliwa na chuo cha CBE ambacho kilijinyakulia kitita cha Sh.300,000.Nafasi
ya tatu ilichukuliwa na chuo cha BMC ambacho kilizawadiwa Sh.200,000 na nafasi
ya nne ni Chuo Kikuu cha TIA ambacho kilipata Sh.100,000.
Kwa upande wa
mchezaji mmoja mmoja (wanaume), Vitalis Bakilane wa CBE aliibuka kuwa bingwa
hivyo kujinyakulia pesa taslimu Sh.150,000 pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa
kwa upande wa wachezaji mmoja mmoja.Nafasi ya pili ilichukuliwa na Joseph
Sipamba wa SAUT ambaye alizawadiwa Sh.100,000.
Na kwa upande wa
mchezaji mmoja mmoja (wanawake), Agnes Jacob wa CBE alitwaa ubingwa huo na
kuzawadiwa pesa taslim sh.100,000 pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa katika
mashindano ya kitaifa.Nafasi ya pili ilichukuliwa na Beatrice Benignus wa TIA
ambaye alizawadiwa pesa taslim Sh 50,000.
Wakati jijini Dar
es Salaam CBE walifanikiwa kumnyang’anya ubingwa wa Mkoa IFM, na kwa nafasi
hiyo CBE ilijinyakulia kitita cha Shilingi 500,000 pamoja na tiketi ya
kushiliki mashindano ya kitaifa . huku nafasi ya pili ikishikiliwa na IFM ambao
walijinyakulia kitita cha Shlingi 300,000.
Nafasi ya tatu
ilichukuliwa na ARDHI ambao walizawadiwa pesa taslimu sh.200,000 na nafasi ya
nne ilichukuliwa na ROYAL ambao walizawadiwa pesa taslimu sh.100,000.
Upande wa wachezaji
mmoja mmoja wanaume Bingwa mtetezi wa Mkoa na Taifa, Peter Patrick wa chuo cha
IFM,alitetea ubingwa wake na kuzawadiwa pesa taslimu sh.150,000 pamoja na
tiketi ya kushiriki mashindano ya kitaifa hapo juni mos jijini Dar es Salaam na
nafasi ya pili ilichukuliwa na Saleh Amir wa IAMCO ambaye alizawadiwa pesa
taslimu sh.100,000,wakati upande wa kinadada nafasi ya kwanza ilichukuliwa na
Lilian Meori na kujinyakula pesa taslimu sh.100,000 na tiketi ya kushiriki
mashindano ya kitaifa wakati nafasi ya pili ilichukuliwa na Mariam Martman na
kujinyakula pesa taslimu sh.50,000.





















