Saturday, December 31, 2011

WACHEZAJI WATIMU YA TAIFA YA NDONDI WAILOTEULIWA KUSHIRIKI KINYANGA"NYIRO CHA KUTAFUTA NAMBA YA KUSHIRIKI OLIMPIKI 2012



Moja ya kambi za mazoezi ya mchezo wa ngumi
KOcha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila Super D akiwa na vifaa vya mchezo hu

Vijana chipukizi wakijifua katika kambi ya mazoezi ya ngumi
Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila Super D akiwa na vifaa vya ngumi
MAJINA YA WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA YA NGUMI WALIOTEULIWA KWA AJIL YA MAANDALIZI YA MASHINDANO YA KUFUZU KWENDA KUWAKILISHA TAIFA KATIKA MASHINDANO YA OLMPIKI LONDON UINGEREZA Julai 2012.


KUTOKA NGOME BOXING TIMU:
1. .SELEMAN KIDUNDA.
2. PETER STANLEY
3. .MORIS MHINA
4. 3.KILLER MOHAMED
5. .ABDALAH KASSIM
6. SUNDAY ELIAS
7. DENIS MARTINE
8. ABDALAH KITENGE
9. HUSSEIN MNIMBO
10. HARUNA SWANGA
11. SAID PUME
12. HASHIM SAIMON
13. RAJABU MADINDA
14. ABDALAH SHABANI
15. ABDU RASHID
16. FRANK NICOLOUS
KUTOKA MMJKT BOXING TIMU:

1. EMILLIAN PATRICK

2. MAXIMILIAN PATRICK
3. ISSA ABDALAH KOBA
4. HAMDAN ISSA
5. SAID HOFU
6. KASSIM HUSSEN
7. BONIFACE MLINGWA
8. DOGO MUSSA
9. GRORGE COSTANTINO
10. JOHN CHRISTIAN
11. VICTOR NJAITI
12. ISMAIL ISACK
13. ELIAS MKOMO
14. WAMBURA AMIRI
KUTOKA MAGEREZA BOXING TIMU:
1. UNDULE LANG"SON

2. NURU IBRAHIM
3. SELEMAN BAMTULA
4. MICHAEL PASCHAL
5. SHABAN ALLY
6. MUSIN KIMWAGA
7. OSWARD CHAULA
8. ANTON IDOA
9. LUSAJO MWAIPOPO
10. MOHAMED CHIBUMBUI
KUTOKA SIFA BOXING TIMU
1. IDDI PIALALI

2. ANCE JOHN
3. SHABAN MAFIGA
4. DOTO SHOKA
KUTOKA POLISI BOXING TIMU
1. YAHAYA MALIKI
KUTOKA URAFIKI BOXING TIMU:
1. FADHIR HASSAN

KUTOKA TEMEKE BOXING TIMU:
1. EDWARD ASAJILE

2. ABDALAH MFAUME
KUTOKA NYAMBELE BOXING TIMU (DODOMA)
1. ANTONY NYAMBELE

KUTOKA MTONI BOXING TIMU
1. CHUKI MOHAMED

NB: MAZOEZI KWA WACHEZAJI 51 WALIOTEULIWA YATAANZA MARA TU BAADA YA KURIPOTI BFT NA KUPANGIWA KITUO CHA KUFANYIA MAZOEZI KATI YA VITUO TULIVYOANISHA VYA UWANJA WA NDANI WA TAIFA,MAGEREZA UKONGA, MGULANI JKT,NGOME,NA URAFIKI.
MWISHONI MWA Januari 2012 KUTAFANYIKA MASHINDANO MAALUM YA MCHUJO KWA HAO WACHEZAJI WALIOTEULIWA ILI KUPATA WACHEZAJI 20.

15-22/2/2012 TIMU HII ITASHIRIKI MASHINDANO YA TAIFA YATAKAYOSHIRIKISHA MIKOA YOTE YA TANZANIA BARA KWA LENGO LA KUSHIRIKISHA MIKOA YOTE ILI TUPATE WAWAKILISHI WA SURA YA KITAIFA.

BAADA YA MCHAKATO HUO NA KURIDHIKA NA WACHEZAJI WALIOFIKIA VIWANGO WATAINGIA KAMBINI KWA AJILI YA MAZOEZI KABAMBE YA MWISHO IKIWA PAMOJA NA KUSHIRIKI MASHINDANO YA MAJARIBIO YA KIMATAIFA KABLA YA KWENDA CASABLANCA MOROCCO KATIKA MASHINDANO YA KUFUZU KWENDA KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.MASHINDANO YA KUFUZU MOROCCO YATAFANYIA KUANZIA TAREHE 27/4-6/5/2012.NA KATIKA MASHINDANO TUNATEGEMEA KUPELEKA WACHEZAJI 10 WA UZITO WA KUANZIA FLY WEIGHT HADI SUPER HEAVY WEIGHT


MAKORE MASHAGA

KATIBU MKUU(BFT)

Mob: +255 713 588818

Email: mashagam@yahoo.com

KIPRE AIONGOZA AZAM KUIUA JKT RUVU CHAMAZI




Kiungo Michael Bolou Kipre wa Azam FC ameiongoza timu yake kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya JKT Ruvu katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo jioni kwenye uwanja wa Azam Chamazi.

Azam FC imepata ushindi huo wa pili mfulilizo katika mechi zake za maandalizi ya ligi kuu na michuano ya Kombe la Mapinduzi, Azam waliifunga Yanga 2-0 kwenye mchezo wake wa kwanza wa kirafiki,

Kipre alikuwa wa kwanza kufungua kalamu hiyo ya magoli katika dakika ya 26 na dakika sita baadaye Khamis Mcha aliifungia klabu hiyo goli la pili na kupeleka timu mapumziko Azam wakiwa mbele kwa 2-0.

Katika mchezo huo uliozikutanishi timu zote zinazocheza ligi kuu ya Vodacom, JKT Ruvu walicheza katika kiwango kizuri na kufanya mchezo kuwa wa kiushindani japo walikuwa nyuma kwa idadi hiyo ya magoli.

Kiungo JKT ruvu kilikuwa chini ya mchezaji Mohamed Banka akishirikiana na wachezaji wengine wa timu hiyo huku Azam FC kulikuwa na Abdi Kassim, Mcha, Salum Aboubakar ‘Sure Boy’ na Kipre walioweza kuichezesha timu hiyo katika kipindi chote cha kwanza.

Kipindi cha pili timu zote ziliongeza kasi na kufanya mabadiliko Azam FC walitoka golikipa Mwadini Ally, Agrey Moris, Waziri Salum, Abdulhalim Humud, Abdi, Kipre na Gaudence Mwaikimba wakaingia golikipa chipukizi Aishi Mfula aliyechukua vyema nafasi hiyo katika dakika ya 72, Luckson Kakolaki, Samir Haji, Abdulghan Gulam, Himid Mao, Zahor Pazi na John Bocco.

Mabadiliko hayo yaliongeza nguvu kwa Azam na kupelekea dakika ya 78 Mcha kupachika goli la tatu baada ya kipa wa JKT Ruvu Amani Simba kupangua shuti la Bocco na mpira huo kumkuta mcha aliyeupeleka wavuni na kumaliza mchezo kwa Azam kupata ushindi huo wa 3-0.

Kocha msaidizi wa Azam, Kali Ongalah amesema ushindi wa mchezo huo ni maandalizi mazuri kwa ajili ya mechi zijazo.

“Tumeshinda huu mchezo wa pili, hatujaruhusu hata goli moja hivyo upande wa ulinzi inaonyesha tupo vizuri na tukiendelea hivi tutafikia malengo yetu” alisema Kali.

Azam FC itaondoka Dar es Salaam siku ya Jumapili kuelekea Zanzibar kwa ajili ya michuano ya Mapinduzi, watacheza mechi ya kwanza siku ya Jumatatu dhidi ya Kikwajuni FC mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Amaan.

WADAU WAOMBWA KUISAIDIA TWIGA STARS





Timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) inaendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam chini ya Kocha Mkuu Charles Boniface Mkwasa kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Namibia baadaye mwezi ujao.
Mechi hiyo ya kwanza itachezwa ugenini Januari 14 mwakani jijini Windhoek. Timu hiyo ambayo sasa inafanya mazoezi kwa wachezaji kutokea majumbani (off camp) inatarajia kuingia kambini Januari Mosi mwakani.
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linahitaji zaidi ya sh. milioni 50 ikiwa ni gharama za safari, kambi na posho kwa wachezaji na benchi la ufundi kwa ajili ya mechi hiyo moja tu. Mechi ya marudiano itachezwa Januari 29 mwakani Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ufunguzi wa Msikiti Donge Muwanda



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya kuufungua Msikiti wa Masjid AL Haramayn Donge Muwanda Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana,(kushoto) Waziri wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati Ali Juma Shamuhuna.
Picha na Ramadhan Othman IKULU.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya kuufungua Msikiti wa Masjid AL Haramayn Donge Muwanda Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana,(kushoto) Waziri wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati Ali Juma Shamuhuna.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akitoa nasaha zake kwa waumini wa Dini ya Kiislamu wakati wa ufunguzi wa Msikiti wa Masjid AL- Haramayn Donge Muwanda, Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana.
Baadhi ya wananchi na viongozi waliohudhurika katika sherehe za ufunguzi wa Msikiti Masjid Al- Haramayn Donge Muwanda uliofunguliwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Friday, December 30, 2011

WADHAMINI WAANZA KUJITOSA KUDHAMINI 'TABORA LIVINGSTONE MARATHON'












Meneja Maendeleo ya Biashara wa Auric Air, Deepesh Gupta (kushoto) akikabidhi msaada wa fulana kwa Mratibu wa mashindano ya mbio za Tabora Livingstone Marathon, Ramadhani Makula jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa mbio hizo, Tullo Chambo.


*************************************************


Na Mwandishi Wetu, jijini


KAMPUNI ya Ndege ya Auric Air ya jijini Dar es Salaam imejitosa kusapoti mashindano ya Mbio ya Tabora Livingstone Marathon yanayotarajiwa kufanyika mjini Tabora Machi mwakani.




Mbio hizo za kwanza katika historia ya Mkoa wa Tabora, zitakuwa za Nusu Marathon Kilomita 21 na zile za kujifurahisha za Kilomita 5.




Akikabidhi msaada wa fulana kwa Mratibu wa mbio hizo, Ramadhani Makula jijini Dar es Salaam jana, Meneja Maendeleo ya Biashara wa Auric Air, Deepesh Gupta, alisema, wamesukumwa kutoa msaada hyo ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu nne chini ya Rais Jakaya Kikwete katika kuendeleza na kuhamasisha michezo hapa nchini.




Gupta alisema, kwa kuzingatia malengo na madhumuni yam bio hizo, wameona japo watoe msaada huo mdogo wa fulana zitakazotumiwa na waratibu na wasimamizi wa mbio hizo ili kusaidia kufanikisha tukio hilo muhimu.




Akipokea msaada huo, Mratibu wa Tabora Livingstone Marathon, Makula, aliishukuru kampuni hiyo na kutoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuwaunga mkono katika kufanikisha mbio hizo za kihistoria.




Makula alisema, hafla ya uzinduzi rasmi wa mbio hizo ambao utawashirikisha wadau na wafadhili mbalimbali utafanyika jijini Dar es Salaam Januari 10.




Aliwataka vijana wenye vipaji mbalimbali wa Mkoa wa Tabora na maeneo ya jirani kujiandaa na mbio hizo, huku akitoa pongezi kwa ushirikiano unaotolewa na Chama cha Riadha Mkoa wa Tabora.

TTCL YAGAWA MISADA MBALIMBALI LEO




Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Bw. Said Amir Said (kushoto) na Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Amin Mbaga (kushoto) wakimkabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa Mkurugenzi wa Kijiji cha SOS kinacholea watoto yatima, Dkt. Alex Lengeju Dare es salaam jana kwa ajili ya sikukuu ya mwaka mpya
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Bw. Said Amir Said (katikati) na Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Amin Mbaga (kulia) wakimkabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa Mratibu wa Maafa Manispaa ya Ilala Bw. Mwasabite Elioth kwa ajili ya watu waliokubwa na mafuriko

RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM KUUAGA MWILI WA ALIYEKUWA MTANGAZAJI WA TBC MAREHEMU HALIMA MCHUKA LEO.






Rais Jakaya Kikwete akipeana mkono na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Bw Clement Mshana wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa mtangazaji Halim Mchuka leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kabla ya kwwenda kuzikwa makaburi ya Msasani baada ya Sala ya Ijumaa. (Picha na Ikulu)


Rais Dk. Jakaya Kikwete pamona na baadhi ya ndugu na watoto wa marehemu wakiuombea dua mwili wa marehemu Halima Mchuka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akitoa heshima za mwisho kuuaga mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) marehemu Halima Mchuka aliyefariki tarehe 29 Desemba mwaka huu jijini Dar es salaam. Mwili wa marehemu umezikwa leo katika makaburi ya Msasani jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)

Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo wakitoa heshima za mwisho kuuaga mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) marehemu Halima Mchuka wakiongozwa na Naibu waziri wa wizara hiyo Dkt. Fennela Mukangara (wa kwanza kulia) katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)


PICHA ZA MWANZO KABISA 2012 HIZI HAPA













































TIGO YASHEREKEA SIKUKUKUU YA CHRISTMAS NA WAKAZI WA MWANZA KATIKA VIWANJA VYA FURAHISHA














Mwanamuziki wa kundi la Top Top Connection Madee akitumbuiza umati katika tamasha maalum la Tigo la kusherehekea sikukukuu za Christmas mjini Mwanza katika viwanja vya Furahisha

WASANII WA AIRTEL BONGO 50 NA PAMOJA NA WAFANYAKAZI WA AIRTEL WATOA POLE NA MSANII WAATHIRIKA WA MAFURIKO DAR ES SALAAM




















Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simuya Airtel ,Jackson Mmbando akizungumza kuhusiana na utoaji wa msaada uliotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-, pichani kati ni Meneja Masoko wa Airtel, Rahma Mwapachu.






Msaani wa filamu/muziki ajulikanae kwa jina kisanii Shilole akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Wasanii wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Flava’ wa Kundi la Wanaume Halisi wakiongozwa na mkali Juma Nature na wakikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko jijini Dar es salaam waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Meneja Masoko wa Airtel, Rahma Mwapaju akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel, Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Msanii mkongwe nchini katika muziki wa Bongo Flava Jafarai akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel, Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Kiongozi wa bendi ya Muziki wa dansi, Ally Choki akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-






Mtayarishaji wa Muziki (Producer) wa Bongo Flava mkongwe P Funk akikabidhi sehemu ya msaada pamoja na umoja wa wasanii wa Airtel Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



SIMBA KUKIPIGA NA MTIBWA SUGAR MCHEZO MAALUM WA KUUAGA NA KUUKARIBISHA MWAKA 2012



Mashabiki wa Simba, wakishangilia katika moja ya mchezo wa timu yao Uwanja wa Taifa.

KLABU ya soka ya Simba itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro katika pambano litakalofanyika katika Uwanja wa Azam, Chamazi jijini Dar es Salaam JIONI ya Jumamosi, Desemba 31 mwaka huu.

Pambano hilo litakuwa la mwisho kwa Simba kucheza jijini Dar es Salaam mwaka huu. Pambano hilo pia litakuwa la mwisho kwa Simba kabla haijakwenda Zanzibar kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyopangwa kuanza Januari 2 mwakani.

Simba itaondoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar Januari Mosi mwaka huu (Jumapili).

Pambano dhidi ya Mtibwa litakuwa sehemu ya maandalizi ya michuano ya Mapinduzi, Ligi Kuu ya Tanzania na michuano ya kimataifa ambayo Simba itashiriki mwakani.

Mechi hiyo itakuwa ya kwanza kwa Kocha Mkuu wa Simba, Profesa Milovan Cirkovic, kukaa kwenye benchi la ufundi na kuiongoza klabu yake hiyo ambayo ni mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi na mabingwa wa kihistoria wa Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati.

Viingilio katika pambano hilo vitakuwa ni Sh 5,000 kwa VIP na 2,000 kwa majukwaa mengine. Simba imeweka kiingilio hicho ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kuhudhuria pambano hilo na kusherehekea kumaliza mwaka salama huku wakiitazama soka la uhakika.

Profesa Cirkovic ameahidi kwamba kwenye pambano hilo atashusha kikosi kamili cha wachezaji wa Simba ili kubaini ni kwa namna gani wachezaji wake wameyaelewa mafunzo yake.

“Nawakaribisha wapenzi na wanachama wa Simba na wapenda soka kwa ujumla waje kwa wingi kuiona Simba ikicheza. Nimesikia kwamba uwanja wa Azam ni mzuri na utaendana na aina ya mchezo ambao Simba itakuwa ikiucheza chini yangu. Nataka kuonyesha soka la asili la Simba,” alisema.

MTANGAZAJI WA TBC TAIFA HALIMA MCHUKA AFARIKI DUNIA



Rais Jakaya Kikwete na mkewe, Mama Salma, wakimjulia hali aliyekuwa mtangazaji wa TBC Taifa, Halima Mchuka wakati wa uhai wake alipokuwa amelazwa hivi karibuni.

Halima amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya jana kuugua ghafla, alipoanza kujisikia vibaya mara tu baada ya kumaliza kipindi cha salam cha mchana na kupelekwa Hospitali.

Kufuatia kifo hicho, KLABU ya soka ya Simba ya Dar es Salaam inatoa salamu za rambirambi kwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na tasnia ya habari kwa ujumla kufuatia kifo cha aliyekuwa mtangazaji maarufu wa michezo nchini, Halima Mchuka, aliyefariki usiku wa kuamkia leo
Jina la Halima Mchuka ni maarufu kwa wanamichezo si Tanzania pekee bali ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati kwa vile yeye aliweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kutangaza mchezo wa soka redioni.
Katika enzi za uhai wake, Halima alifanya kazi kwa karibu na klabu ya Simba, akitembelea ofisi za makao makuu mtaa wa Msimbazi kwa ajili ya kutafuta taarifa mbalimbali za kimichezo.

Simba itaukumbuka daima mchango wa Halima Mchuka kama mwanahabari, mwanamichezo na mtu ambaye alivutia wanawake wengi kupenda mchezo wa soka na pia kazi ya utangazaji na uandishi wa habari kwa ujumla.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi. Amen.

Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga Ofisa Habari
Simba Sports Club
0772 01 72 47

Thursday, December 29, 2011

SUPER D BOXING COACH KUENDELEA KUWANOA VIJANA ZAIDI 2012




Super D Boxing Coach kushoto akiwa katika moja ya GYM


super D Boxing Coach





Super D Boxing Coach Akiwa na Talik Balozi wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Ilala





mazoezi ni Afya akisisitiza Super D Boxing Coach




Super D Boxing Coach akiwa na mwanae Ikota anaefuata nyayo za masumbwi




Na Mwandishi WetuALIYEKUWA bondia wa ngumi za kulipwa Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye pia ni kocha wa timu ya ngumi ya Ashanti Ilala amesema anajivunia mafanikio makubwa aliyoyapata katika mchezo wa ngumi katika kipindi cha mwaka 2011.Akizungumza na waandishi wa habari Super D ambaye pia ni mpiga picha wa Magazeti ya Busines Time, Majira, Sports Starehe na jarida la Maisha alisema moja ya mafanikio ni kuwaandaa vijana chipukizi wengi na kuwafikisha katika kiwango kizuri cha kuvuna matuna ya mchezo huo.Alisema pamoja na hilo pia ameweza kushirikiana vema na wadau wa ngumi pamoja na mapromota mbalimbali wanaoandaa mapambano makubwa kwa kutoa mchango wake wa vifaa vya ngumi ili kufanikisha mapambano mbalimbali yaliyofanyika katika kipindi cha mwaka huu.Katika hatua nyingine Super D amekua akitoa mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria mbalimbali kwa njia ya DVD zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khanny, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi.Alisema mipango yake kwa mwaka 2012 ni kuhakikisha anaendelea kuwainua mabondia wengine chipkizi akiwemo bondia Shomari Mirundi na Ibrahimu Class ambao amewataja ni mabondia wazuri wanaohitaji kuendelezwa vipaji vyao.Alisema bondia Ubwa Salum ambaye alimtwanga Mustapha Doto,kwa pointi 60-57 alishinda ambapo pambano hilo lilikuwa moja ya mapambano ya utangulizi ya pambano kubwa la Rashidi Matumla na Maneno Osward lililofanyika DEsemba 25 mwaka huu.
Superd Boxing Coach

Wednesday, December 28, 2011

NETIBOLI HIYO ZANZIBAR KUSHIRIKI KOMBE LA MAPINDUZI













T



Timu ya netiboli inayounda kikosi cha timu ya Taifa inaondoka kesho kuelekea visiwani ZANZIBAR kushiriki mashindano ya kombe la Mapinduzi ambapo kikosi hicho kitakuwa chini ya kocha MARY PROTAS na kocha kutoka TANZANIA VISIWANI.





Baadhi ya timu zilizoambwa kushiriki mashindano hayo ni ZAMBIA, BOTSWANA, MALAWI, NAMIBIA ,KENYA na UGANDA.





Mjumbe wa kamati ya utendaji wa CHANETA MWAJUMA KISENGO amesema timu hiyo itafanya vizuri kwani ndiyo timu iliyoshiriki mashindano ya ALL AFRICANS GAME nchini MSUMBIJI.

Hamad rashid agoma kuhojiwa na kamati ya mahadil cuf

























Raymond Kaminyoge na Aziza Masoud


HALI bado tete ndani ya Chama Cha Wananchi (CUF) baada ya Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed, kugoma kuhojiwa na Kamati ya Nidhamu na Maadili ya chama hicho kuhusu tuhuma za kuvunja katiba. Mbunge huyo aliibua tuhuma nzito kwamba amekamata waraka wa siri wa viongozi wawili waandamizi wa chama hicho, waliokuwa wakipanga njama za kumfukuza.





Hamad aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa ana sababu tano za kugomea kikao hicho, ambazo ni pamoja na waraka huo wa siri aliodai ulitoka kwa mmoja wa viongozi hao kwenda kwa mwenzake. Waraka huo ambao Hamad alidai kuunasa unasomeka, “Tuwe waangalifu tusiingie katika mtego” na uliandikwa Desemba 14 2011 na kutumwa kwa barua pepe.





“ …anataka nifukuzwe kwenye chama, baadhi walioteua na walioteuliwa katika Kamati ya Nidhamu na Maadili wamekwishanituhumu hadharani na kunitia hatiani hivyo kikao hiki hakitatenda haki,” alisema Hamad.





Alitaja sababu nyingine ya kukataa kuhojiwa kuwa ni kutoelezwa tuhuma zake hasa vifungu vya Katiba alivyodaiwa kuvikiuka. “ Ni vema nikaelezwa ni vifungu vipi vya katiba hiyo nilivyokwenda navyo kinyume,” alisema Hamad. Alifafanua kwamba, alitaka apewe hadidu za rejea za kikao kilichounda Kamati ya Nidhamu na Maadili kwa sababu kikatiba, hakuna chombo kama hicho.





“Katiba ya CUF haina chombo kama hicho, kamati hii imeundwa na nani nikipewa hadidu za rejea za kikao kilichounda kamati hiyo zitanisaidia katika kumbukumbu,” alisema Hamad Rashid. Alisema alitaka pia apewe nakala ya uteuzi wa wajumbe walioteuliwa katika kamati hiyo.





Mbunge huyo pia alisema amegomea kikao hicho hadi atakapopewa kanuni zitakazotumika katika kuendesha shughuli nzima ya kujibu tuhuma hizo na kupewa katiba iliyotumika ambayo ameivunja. “Nataka kupewa vitu hivyo ili niweze kuweka kumbukumbu sahihi kwa kila hatua inayochukuliwa na chama,” alisema mbunge huyo wa CUF.





Akizungumzia kamati hiyo, mbunge huyo alisema kati ya wajumbe wanane, watano hana imani nao kwa sababu wamekuwa wakimtuhumu hadharani. “Hawa wajumbe sina imani nao uamuzi wao hautakuwa wa haki,” alisema Hamad. Juzi Hamad Rashid na wenzake 13 waliitwa na Kamati na Nidhamu ili kujibu tuhuma za kuvunja Katiba ya chama hicho. Hatua hiyo imekuja baada ya mvutano wa muda mrefu kati ya Katibu Mkuu na Mbunge huyo kutuhumiana hadharani.





Waraka wa Siri


Hamad alisema hawezi kuhudhuria kikao hicho kwa kuwa tayari amebaini njama za kushughulikiwa zilizosukwa na vigogo wawili wa chama hicho dhidi yake.“ Nimeshauriana na Makamu na tumeona kuna haja ya jamaa yako (Rashid) na genge lake kuitwa katika Kamati ya Nidhamu na Maadili kuhojiwa,” inasema sehemu ya waraka huo ambao aliusambaza kwa vyombo vya habari.





Waraka huo uliongeza, “ushahidi wa kutosha umekusanywa dhidi yake na wasaidizi wake wakuu na muono wetu ni kuwa tumfukuze uanachama.” Waraka huo ulisisitiza, “Wanachama walio wengi wanatudadisi kwa nini hatuchukui hatua, akishajulikana kuwa si mwanachama atakuwa hana mashiko muache aende CCM au Chadema.” Alipoulizwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Nidhamu wa CUF, Abdul Kambaya alisema taarifa za Rashid kukataa kuhojiwa na Kamati zitapelekwa katika Kamati ya Utendaji.





“ Ni kweli Hamad amegoma kuhojiwa kuhusu tuhuma zinazomkabili, lakini tunachofanya ni kupeleka taarifa kwa kamati ya Utendaji itakayofanya maamuzi,”alisema Kambaya na kubainisha kuwa kamati hiyo inaendelea kuwahoji wanachama wengine wanaotuhumiwa kuvunja katiba ya chama hicho.





Hivi karibuni Hamad Rashid alijikuta kwenye mgogoro na baadhi ya viongozi wa makao makuu ya chama hicho, baada ya kutangaza dhamira hiyo yake ya kugombea nafasi ya katiba mkuu mwaka 2014. Kuanzia hapo akajikuta ameingia kwenye mgogoro na chama hicho kiasi cha kunusurika kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati akigawa misaada katika matawi ya chama hicho, kata ya Manzese. Mvutano huo ulisababisha vurugu katika tawi la Chechnya ambako wanachama wanaomuunga mkono walipambana na walinzi wa Blue Guard na kusababisha umwagaji damu.www.mwananchi.co.tz

Rais Dk. Shein ashiriki katika mazishi ya marehemu Kanali Nassor Waziri Mageta
















Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia) pamoja na Viongozi wengine wakiusalia mwili wa Marehemu Kanal Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia,katika msikiti masjid Twariq Bububu nje wa mji wa Zanzibar, aliyefariki jana na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni Wilaya Magharibi Unguja wakilibeba jeneza la Marehemu Kanal Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia,aliyefariki jana na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Askari wa Vikosi vya SMZ,wakilibeba Jeneza lenye mwili wa Marehemu Kanal Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia,aliyezikwa jana katika kijiji cha mkanyageni Wilaya ya Magharibi mkoa wa mjini magharibi Unguja.


Askari wa Vikosi vya SMZ wakiondoa Nguo alizozitumia marehemu Kanali Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia, aliyefariki jana na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,( katikati) pamoja na Viongozi wengine wakiwa katika maziko ya Marehemu Kanal Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia, aliyefariki jana na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,akitia udongo katika kaburi la Marehemu Kanal Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia,aliyefariki leo na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Askari wa Vikosi vya SMZ wakitoa salamu ya hesha katika kaburi la marehemu Kanali Nassor Waziri Mageta,aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia, aliyefariki jana na kuzikwa Kijiji kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja. Picha na Ramadhan Othman IKULU